01. MWOKOZI UMEOKOA

MWOKOZI UMEOKOA

1.  Mwokozi umeokoa,
Nimekuwa wako wewe.
Damu imenisafisha;
Sifa kwa mwana Kondoo.

Chorus:
Utukufu, Aleluya!
Sifa kwa Mwana Kondoo!
Damu imenisafisha,
Utukufu kwa Yesu!
 
2.  Nilijitahidi sana
Ila sikupata raha;
Bali kwa kumtegemea
Nilipata baraka.
 
3.  Daima namwegemea,
Damu ikifanya kazi,
Nikioga kwa chemchemi
Itokayo Mwokozi.
 
4.  Sasa nimewekwa wakfu;
Nitaishi kwako Wewe:
Fahari nashuhudia
Ya wokovu wa bure.
 
5.  Nasimama kwake Yesu,
Ameponya roho yangu;
Ameniondoa dhambi,
Anifanye mzima.
 
6.  Nilikuwa kifungoni,
Niliteswa na dhambi,
Nilifungwa minyororo
Yesu akanifungua.
 
7.  Sifa, ameninunua!
Sifa, nguvu za wokovu!
Sifa, Bwana huhifadhi!
Sifa zake milele.

Comments