Posts

Showing posts from March, 2022

01. MWOKOZI UMEOKOA

MWOKOZI UMEOKOA 1.    Mwokozi umeokoa, Nimekuwa wako wewe. Damu imenisafisha; Sifa kwa mwana Kondoo. Chorus: Utukufu, Aleluya! Sifa kwa Mwana Kondoo! Damu imenisafisha, Utukufu kwa Yesu!   2.    Nilijitahidi sana Ila sikupata raha; Bali kwa kumtegemea Nilipata baraka.   3.    Daima namwegemea, Damu ikifanya kazi, Nikioga kwa chemchemi Itokayo Mwokozi.   4.    Sasa nimewekwa wakfu; Nitaishi kwako Wewe: Fahari nashuhudia Ya wokovu wa bure.   5.    Nasimama kwake Yesu, Ameponya roho yangu; Ameniondoa dhambi, Anifanye mzima.   6.    Nilikuwa kifungoni, Niliteswa na dhambi, Nilifungwa minyororo Yesu akanifungua.   7.    Sifa, ameninunua! Sifa, nguvu za wokovu! Sifa, Bwana huhifadhi! Sifa zake milele.

02. TWAMSIFU MUNGU

TWAMSIFU MUNGU 1.    Twamsifu Mungu kwa Mwana wa pendo, Aliyetufia na kupaa juu. Chorus: Aleluya! Usifiwe, Aleluya! Amin. Aleluya! Usifiwe, utubariki.   2.    Twamsifu Mungu kwa Roho Mtukufu, Ametufunulia Mwokozi wetu.   3.    Twamsifu Mwana, aliyetufia, Aliyetwaa dhambi akazifuta.   4.    Twamsifu Mungu wa neema yote, Ametukomboa akatuongoza.   5.    Tuamshe tena, tujaze na pendo, Na moyoni uwashe moto wa Roho.

03. HATA NDIMI ELFU

HATA NDIMI ELFU 1.    Hata ndimi elfu elfu, Hazitoshi kweli Bwana Yesu kumsifu, Kwa zake fadhili.   2.    Yesu, jina liwezalo Kufunza hofu; Lanifurahisha hilo, Lanipa wokovu.   3.    Jina hilo ni uzima; Ni afya; amani; Laleta habari njema; Twalipiwa deni.   4.    Yesu huvunja mapingu Ya dhambi moyoni; Msamaha, tena nguvu, Twapata rohoni.   5.    Kwa sauti yake vile Wafu hufufuka Wakafurahi milele, Pasipo mashaka.   6.    Ewe Yesu wangu Bwana, Uwezo nipewe, Kuhubiri kote sana, Wote wakujue.

04. JINA LA YESU, SALAMU!

JINA LA YESU, SALAMU! 1.    Jina la Yesu, salamu! Lisujudieni, Ninyi Mbinguni, hukumu Na enzi mpeni.   2.    Enzi na apewe kwenu, Watetea dini; Mkuzeni Bwana wenu, Na enzi mpeni.   3.    Enyi mbegu ya rehema, Nanyi msifuni; Mmeponywa kwa neema, Na enzi mpeni.   4.    Wenye dhambi kumbukeni Ya Msalabani, Kwa furaha msifuni, Na enzi mpeni.   5.    Kila mtu duniani Msujudieni, Kotekote msifuni, Na enzi mpeni.   6.    Sisi na wao pamoja Tu mumo sifani, Milele sifa ni moja, Ni “Enzi mpeni.”

05. JINA LAKE YESU TAMU

JINA LAKE YESU TAMU 1.    Jina lake Yesu tamu; Tukilisikia Hutupoza, tena hamu Hutuondolea.   2.    Roho iliyoumia Kwalo hutibika, Chakula, njaani pia; Raha, tukichoka.   3.    Jina hili ni msingi, Ngao, ngome, mwamba, Kwa hili napata wingi, Kwangu ni akiba.   4.    Yesu, Mchunga, Rafiki, Mwalimu, Kuhani, Mwanzo, Mwisho, Njia, Haki. Uzima kifoni.   5.    Moyo wangu hauwezi Kukusifu kweli, Ila sifa zangu hizi, Bwana zikubali.   6.    Na utakaponiita, Kuja kwako Bwana, Huko kwako sitaacha Kukusifu sana.

06. MUNGU MWENYE ENZI

MUNGU MWENYE ENZI   1.    Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi. Kila tukiamka tunakuabudu Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi, Ewe Utatu, tunakusifu.   2.    Baba, Mwana, Roho, wakuaminio Wanakutolea shukurani zao. Wanakusujudia malaika nao; Wewe u mwanzo, nawe u mwisho.   3.    Baba, Mwana, Roho, sisi tu gizani, Utukufu wako hauoni kosa; U Mtakatifu, nawe u mapenzi, U peke yako, mwenzio huna.   4.    Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi, Ulivyoviumba vyote vyakusifu; Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi Ewe Utatu, tunakusifu.

07. NI TABIBU WA KARIBU

NI TABIBU WA KARIBU 1.    Ni tabibu wa karibu; Tabibu wa ajabu; Na rehema za daima; Ni dawa yake njema.   Chorus: Imbeni, malaika, Sifa za Yesu Bwana; Pweke limetukuka Jina lake Yesu.   2.    Hatufai kuwa hai, Wala hatutumai, Ila Yeye kweli ndiye Atupumzishaye.   3.    Dhambi pia na hatia Ametuchukulia; Twenendeni na amani Hata kwake Mbinguni.   4.    Huliona tamu jina La Yesu Kristo Bwana, Yuna sifa mwenye kufa Asishindwe na kufa.   5.    Kila mume asimame, Sifa zake zivume; Wanawake na washike Kusifu jina lake.   6.    Na vijana wote tena, Wampendao sana Waje kwake wawe wake Kwa utumishi wake.

08. TAJI MVIKENI

TAJI MVIKENI 1.    Taji mvikeni, Taji nyingi tena, Kondoo mwake Kitini, Bwana wa mabwana; Nami tamsifu Alikufa kwangu, Ni mfalme mtukufu, Mkuu wa Mbingu.   2.    Taji mvikeni Mwana wa bikira; Anazovaa kichwani Aliteka nyara; Shiloh wa manabii, Mchunga wa watu, Shina na tanzu vya Yesu, Wa Bethilehemu.   3.    Taji mvikeni Bwana wa mapenzi; Jeraha zake ni shani Ni vito vya enzi, Mbinguni hakuna Hata malaika Awezaye kuziona Pasipo kushangaa.

09. YESU KWETU NI RAFIKI

YESU KWETU NI RAFIKI 1.    Yesu kwetu ni rafiki, Hwamiwa haja pia; Tukiomba kwa Babaye Maombi asikia; Lakini twajikosesha, Twajitweka vibaya; Kwamba tulimwomba Mungu Dua angesikia.   2.    Una dhiki na maonjo? Una mashaka pia? Haifai kufa moyo, Dua atasikia Hakuna mwingine mwema Wa kutuhurumia; Atujua tu dhaifu; Maombi asikia.   3.    Je, hunayo hata nguvu, Huwezi kwendelea, Ujapodharauliwa Ujaporushwa pia. Watu wangekudharau, Wapendao dunia, Hukwambata mikononi, Dua atasikia.

10. USINIPITE MWOKOZI

USINIPITE MWOKOZI 1.    Usinipite Mwokozi, Unisikie; Unapozuru wengine, Usinipite.   Chorus: Yesu,Yesu, Unisikie; Unapozuru wengine, Usinipite.   2.    Kiti chako cha rehema, Nakitazama; Magoti napiga pale, Nisamehewe.   3.    Sina cha kutegemea, Ila Wewe tu; Uso wako uwe kwangu; Nakuabudu.   4.    U Mfariji peke yako; Sina Mbinguni, Wala duniani pote, Bwana mwingine.

11. NINA HAJA NAWE

NINA HAJA NAWE 1.    Nina haja nawe Kila saa; Hawezi mwingine Kunifaa. Chorus: Yesu, nakuhitaji Vivyo kila saa! Niwezeshe, Mwokozi, Nakujia.   2.    Nina haja nawe; Kaa nami, Na maonjo haya, Hayaumi.   3.    Nina haja nawe; Kila hali, Maisha ni bure, Uli mbali.   4.    Nina haja nawe, Nifundishe Na ahadi zako Zifikishe.   5.    Nina haja nawe, Mweza yote, Ni wako kabisa Siku zote.